Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Mkuu
 wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telak akizungumza na watalaamu pamoja na 
wadau wa uhifadhi walioshiriki jana kwenye  kongamano ambalo lilikuwa ni
 sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ambayo Kitaifa 
inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu.
 Mkurugenzi
 wa Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa akijibu hoja 
zilizotolewa na wadau mbalimbali  wa uhifadhi wa Misitu jana  wakati wa 
kongamano ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji 
miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu
 
 Mdau
 wa Uhifadhi wa Mazingira, Anna Matinye akichangia hoja  jana kwenye 
kongamano ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji 
miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu.
 Mkurugenzi
 wa Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa akiwasilisha 
maada   kwa wadau mbalimbali  wa uhifadhi wa Misitu kwa kuwasomea baadhi
 ya vipengele kwenye kitabu cha Sera ya Taifa ya Misitu  jana wakati wa 
kongamano ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji 
miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu
 Meneja
 wa Kanda ya Magharibi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) 
Valentine Msusa  akijibu baadhi ya hoja za wadau kwenye kongamano ambalo
 lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ambayo 
Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu
 Mkuu
 wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telak ( wa tatu kushoto)  akiwa 
ameambatana na Kamati ya ulinzi na usalama wakiangalia baadhi ya miti 
iliyopandwa katika Shule ya Sekondari ya Kishapu inavyoendelea vizuri 
kabla ya kuanza kwa kongamano lililofanyika jana  ambalo lilikuwa ni 
sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ambayo Kitaifa inafanyika
 Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu
 Mkurugenzi
 wa Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa ( watatu kushoto) 
akiwa pamoja  na Mkurugenzi wa Rasilimali Misitu wa Wakala wa Huduma za 
Misitu Tanzania (TFS) Zawadi Mbwambo ( wapili kushoto) wakiandika 
baadhi  hoja zinazowatolewa na  wadau mbalimbali  wa uhifadhi wa Misitu 
 wakati wa kongamano ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya
 upandaji miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani 
Kishapu
 Baadhi
 ya wadau wa uhifadhi wa Mazingira na Misitu wakifuatilia kongamano 
lililofanyika jana  ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya 
upandaji miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani 
Kishapu

 
Mdau
 wa Uhifadhi wa Mazingira, Modestus Nyenza  akichangia hoja jana  kwenye
 kongamano ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji 
miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu.
Na Lusungu Helela-Shinyanga
Mkuu
 wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telak amewatahadhalisha wananchi kuwa 
yeyote atakayeharibu misitu kwa kukata au kuingiza mifugo kwenye  misitu
 atachukuliwa hatua za kisheria.
Akizungumza
 jana wilayani Kishapu  wakati wa  kongamano ambalo lilikuwa ni sehemu 
ya maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani
 humo,  Mkuu wa Mkoa  alipiga marufuku kukata miti bila ruhusa yake au 
ya Mkuu wa wilaya. 
Telak
 alisema marufu hiyo imekuja kwa kuchelewa kwa vile hatua iliyofikia  
katika Wilaya hiyo  inatisha  hakuna mahindi yanayostawi kutokana  na  
kutokuwa na  mvua ya kutosha. 
‘’Mtu yeyote atakayekata miti ajiandae kupelekwa jela  kwa vile kukata miti katika wilaya hii ni sawa na uuaji.’’ alisema Telak
Alifafanua
 kuwa mtu yeyote atakayetaka kukata miti hata ule uliopo uwanjani pake 
ni lazima aombe kibali kwa wahusika na atakayekiuka kukata bila kibali 
ajue jela inamwita.
 Wakati
 huo huo, Telak  alitoa agizo kwa wakuu wa wilaya wote kuhakikisha 
wanawakamata wale wote  watakaoingiza mifugo kwenye maeneo yaliyopandwa 
miti.
Aliongeza
 kuwa uharibifu wa misitu  unaoendelea kufanyika katika maeneo hayo  
unazidi kuathiri hata  mifugo  kutokana na kukosekana kwa malisho kwa 
vile hakuna mvua inayonyesha.
Kwa
 upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Ezekiel 
Mwakalukwa  alisema suala la kulinda misitu linahitaji ushirikiano 
kutoka kwa jamii, wizara pekee haiwezi.
Alisema
 tatizo la uharibifu wa misitu katika wilaya ya Kishapu limechochea 
Idara kutengeneza kanzidata itakayosaidia kuzibana Halmashauri kujua 
imepanda miti mingapi na kati ya hiyo mingapi imepona. 
‘’Tunaanza  mwaka huu kukagua  ili kujua miti hiyo imepandwa wapi na maendeleo yake yakoje’’  alisisitiza  Mwakalukwa.
Amesema
 hali hiyo itasaidia kuthibiti Halmashauri ambazo zimekuwa zikitaja 
idadi kubwa ya miti iliyopandwa kila mwaka lakini miti hiyo imekuwa 
haionekani ikikua na pale unapohitaji kupelekwa ukaone miti hiyo  
visingizio lukuki vimekuwa vikiibuka.
Maadhimisho
 ya wiki ya upandaji miti Kitaifa yanafanyika Wilayani Kishapu Mkoani 
Shinyanga ambapo kauli mbinu yake ni Tanzania ya kijani inawezekana 
panda miti kwa maendeleo ya viwanda