MAADHIMISHO YA UPANDAJI MITI KITAIFA SHINYANGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 

RC SHINYANGA AWATAHADHALISHA WAHARIBIFU WA MISITU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telak akizungumza na watalaamu pamoja na wadau wa uhifadhi walioshiriki jana kwenye  kongamano ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu.
 Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa akijibu hoja zilizotolewa na wadau mbalimbali  wa uhifadhi wa Misitu jana  wakati wa kongamano ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu
 Mdau wa Uhifadhi wa Mazingira, Anna Matinye akichangia hoja  jana kwenye kongamano ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu.
 Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa akiwasilisha maada   kwa wadau mbalimbali  wa uhifadhi wa Misitu kwa kuwasomea baadhi ya vipengele kwenye kitabu cha Sera ya Taifa ya Misitu  jana wakati wa kongamano ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu
 Meneja wa Kanda ya Magharibi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Valentine Msusa  akijibu baadhi ya hoja za wadau kwenye kongamano ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu
 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telak ( wa tatu kushoto)  akiwa ameambatana na Kamati ya ulinzi na usalama wakiangalia baadhi ya miti iliyopandwa katika Shule ya Sekondari ya Kishapu inavyoendelea vizuri kabla ya kuanza kwa kongamano lililofanyika jana  ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu
 Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa ( watatu kushoto) akiwa pamoja  na Mkurugenzi wa Rasilimali Misitu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Zawadi Mbwambo ( wapili kushoto) wakiandika baadhi  hoja zinazowatolewa na  wadau mbalimbali  wa uhifadhi wa Misitu  wakati wa kongamano ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu
 Baadhi ya wadau wa uhifadhi wa Mazingira na Misitu wakifuatilia kongamano lililofanyika jana  ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu
Mdau wa Uhifadhi wa Mazingira, Modestus Nyenza  akichangia hoja jana  kwenye kongamano ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani Shinyanga wilayani Kishapu.
Na Lusungu Helela-Shinyanga
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telak amewatahadhalisha wananchi kuwa yeyote atakayeharibu misitu kwa kukata au kuingiza mifugo kwenye  misitu atachukuliwa hatua za kisheria.
Akizungumza jana wilayani Kishapu  wakati wa  kongamano ambalo lilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ambayo Kitaifa inafanyika Mkoani humo,  Mkuu wa Mkoa  alipiga marufuku kukata miti bila ruhusa yake au ya Mkuu wa wilaya. 
Telak alisema marufu hiyo imekuja kwa kuchelewa kwa vile hatua iliyofikia  katika Wilaya hiyo  inatisha  hakuna mahindi yanayostawi kutokana  na  kutokuwa na  mvua ya kutosha. 
‘’Mtu yeyote atakayekata miti ajiandae kupelekwa jela  kwa vile kukata miti katika wilaya hii ni sawa na uuaji.’’ alisema Telak
Alifafanua kuwa mtu yeyote atakayetaka kukata miti hata ule uliopo uwanjani pake ni lazima aombe kibali kwa wahusika na atakayekiuka kukata bila kibali ajue jela inamwita.
 Wakati huo huo, Telak  alitoa agizo kwa wakuu wa wilaya wote kuhakikisha wanawakamata wale wote  watakaoingiza mifugo kwenye maeneo yaliyopandwa miti.
Aliongeza kuwa uharibifu wa misitu  unaoendelea kufanyika katika maeneo hayo  unazidi kuathiri hata  mifugo  kutokana na kukosekana kwa malisho kwa vile hakuna mvua inayonyesha.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Ezekiel Mwakalukwa  alisema suala la kulinda misitu linahitaji ushirikiano kutoka kwa jamii, wizara pekee haiwezi.
Alisema tatizo la uharibifu wa misitu katika wilaya ya Kishapu limechochea Idara kutengeneza kanzidata itakayosaidia kuzibana Halmashauri kujua imepanda miti mingapi na kati ya hiyo mingapi imepona. 
‘’Tunaanza  mwaka huu kukagua  ili kujua miti hiyo imepandwa wapi na maendeleo yake yakoje’’  alisisitiza  Mwakalukwa.
Amesema hali hiyo itasaidia kuthibiti Halmashauri ambazo zimekuwa zikitaja idadi kubwa ya miti iliyopandwa kila mwaka lakini miti hiyo imekuwa haionekani ikikua na pale unapohitaji kupelekwa ukaone miti hiyo  visingizio lukuki vimekuwa vikiibuka.

Maadhimisho ya wiki ya upandaji miti Kitaifa yanafanyika Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga ambapo kauli mbinu yake ni Tanzania ya kijani inawezekana panda miti kwa maendeleo ya viwanda

WAZIRI KIGWANGALLA KUONGOZA KILELE CHA MAADHIMISHO YA UPANDAJI MITI KITAIFA KESHO MKOANI SHINYANGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

DC MATIRO APIGISHA KURA ZA SIRI KUBAINI WAUAJI WA WANAWAKE SHINYANGA VIJIJINI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Wananchi wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiwasisitiza wananchi kutoa ushirikiano katika vyombo vya sheria ili kukomesha mauaji katika kata ya Salawe
Wananchi wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Shinyanga

Na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Kufuatia kuibuka kwa taarifa za kuwepo kwa mauaji ya wanawake yanayoambatana na imani za kishirikina katika kata ya Salawe wilaya ya Shinyanga, mkuu wa wilaya hiyo Josephine Matiro amefanya mkutano na wananchi wa eneo hilo kwa ajili ya kutafuta chanzo na ufumbuzi kumaliza mauaji hayo.

Wananchi wa kijiji cha Songambele kata ya Salawe wanasema mauaji hayo yameanza kutokea tangu mwezi Desemba mwaka jana wakidai kuwa wanawake hukatwa mapanga ama kunyongwa na watu wasiofahamika ambao hutoweka na viungo vya siri vya wanawake wanaowaua. 

Inaelezwa kuwa katika kipindi cha  Januari Mosi hadi Machi 23 mwaka huu watu waliouawa katika kata hiyo ni wanne huku mauaji hayo yakihusishwa na imani za kishirikina.Kutokana na hali hiyo Mkuu wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya hiyo, alifika katika kata ya Salawe kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi wa mauaji hayo kwa njia ya kuwashirikisha wananchi.

Aidha baada ya kuzungumza na wananchi wa eneo hilo katika mkutano wa hadhara,mkuu huyo wa wilaya aliagiza kufanyika/kupigwa kwa kura za maoni kwa ajili ya kuwabaini wahusika wa mauaji hayo na kuondoka na kura hizo kwa ajili ya kuzifanyia kazi.

“Katika wilaya ya Shinyanga kuna kata 43, matukio ya mauaji ya namna hii yanatokea hapa,ni nyinyi hapa tu,sasa tumtafute mchawi na tumfanyie kazi,mkitaka kulimaliza tatizo hili ni  lazima mtupe ushirikiano,muwe tayari kufika mahakamani pale mtakapohitajika ,mjitokeze kutoa ushahidi ili wale watu msiwaone tena kwenye mitaa yenu”,alisema Matiro.

“Wananchi mmeendelea kulalamika kuwa kuna mauaji na kuitupia lawama serikali wakiwemo askari polisi kuwa wanapokea rushwa na kuwaachia huru watuhumiwa kumbe tatizo ni nyinyi kutotoa ushirikiano,naomba mbadilike, wafichueni wahusika ili tukomeshe tatizo hili kwani tunataka watu wawe salama na waishi kwa amani”,alieleza Matiro.

Aidha aliwataka viongozi wa serikali za mitaa na wananchi kwa ujumla kuacha kupokea wageni na kwamba wageni wote wajitambulishe ili kujua wanafanya nini na wametoka wapi ili kukomesha
Wakizungumza mbele ya mkuu wa wilaya ya Shinyanga, wananchi hao walisema matukio hayo yanatishia usalama wao na kusababisha waishi kwa hofu.

Walisema mbali na kuishi kwa hofu pia wanashindwa kufanya kazi zao za maendeleo na uzalishaji mali.Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga, ACP Simon Haule aliyekiri kuwepo kwa mauaji katika kata ya Salawe alisema chanzo ni kuwania mali,migogoro ya mashamba,wivu wa mapenzi na imani za kishirikina.

Aidha aliwataka wananchi kupuuza uzushi kwamba kwenye kata hiyo kuwa kuna watu wanakata mapanga wanawake na kisha kuondoka na sehemu zao nyeti yakiwemo matiti. 

“Kwenye mkoa wa Shinyanga hakuna kitu kama hicho, isipokuwa kuna takwimu za wananchi 27 kuuawa kwa kukatwa mapanga kutokana na sababu mbalimbali kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo kuanzia (2016- Machi 2018) ambapo wanawake 12, na wanaume 15. 

Alitaja takwimu za mauaji mkoa wa Shinyanga kwa kuchambua kila mwaka ambapo mwaka (2016) waliuawa watu 12, wanawake Sita, Wanaume Sita, (2017) wanaume nane, wanawake wanne, mwaka huu (2018) kuanzia Januari hadi Machi wanawake wawili na mwanaume mmoja jumla watu 27. 

RC TELACK AWASILISHA KILIO CHA UMEME KWA WAZIRI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Subira Mgalu akitoa salamu kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack wakati alipomtembelea Ofisini kwake mapema leo.
 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akizungumza na Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Subira Mgalu na msafara wake, Ofisini kwake mapema leo.

MGODI WA EL HILLARY WAPEWA SIKU 14 KUJISAJILI MFUKO WA FIDIA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana Mhe. Antony Mavunde akitoa salam kwa uongozi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Shinyanga mara baada ya kuwasili Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Shinyanga. Kushoto aliyekaa ni Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dotto Biteko ambaye wameongozana katika ziara hiyo.
 Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana Mhe. Antony Mavunde (kushoto), Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dotto Biteko (kulia) wakiwa Ofisini kwa Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Josephine Matiro walipofika kwa ajili ya kusaini kitabu cha wageni mapema jana.
 Naibu Waziri Mhe. Mavunde akitembelea mgodi wa almasi wa El Hillary baada ya kutoa maelekezo katika ziara yake mgodini hapo.

 Naibu Mawaziri wa Kazi, Ajira na Vijana Mhe. Antony Mavunde (wa pili kushoto) na Madini Mhe. Dotto Biteko (katikati) wakitoa maelekezo kwa uongozi wa El Hillary mapema jana wakati wa ziara yao ya pamoja mgodini hapo.


NAIBU WAZIRI DK. NDUGULILE AFANYA ZIARA WILAYA YA SHINYANGA KUKAGUA HUDUMA ZA AFYA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amepiga marufuku dawa za serikali kuonekana zikiuzwa kwenye maduka ya watu binafsi kwani serikali haitaki kuingia kwenye matatizo ya uhaba wa dawa kwenye sehemu zake za kutolewa huduma ya afya.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa