Home » » NAIBU WAZIRI DK. NDUGULILE AFANYA ZIARA WILAYA YA SHINYANGA KUKAGUA HUDUMA ZA AFYA

NAIBU WAZIRI DK. NDUGULILE AFANYA ZIARA WILAYA YA SHINYANGA KUKAGUA HUDUMA ZA AFYA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amepiga marufuku dawa za serikali kuonekana zikiuzwa kwenye maduka ya watu binafsi kwani serikali haitaki kuingia kwenye matatizo ya uhaba wa dawa kwenye sehemu zake za kutolewa huduma ya afya.
Dk. Ndugulile amepiga marufuku dawa za serikali kuonekana zikiuzwa kwenye maduka ya watu binafsi wakati wa ziara yake ya kikazi katika wilaya ya Shinyanga, Februari 21,2018 akikagua shughuli za huduma za afya zinavyotolewa kwa wananchi pamoja na kutoa hamasa kwa jamii kujiunga na Bima ya afya ya jamii CHF iliyoboreshwa.
Dk. Ndugulile alisema katika bajeti ya mwaka wa fedha (2017-18) serikali kwenye bajeti ya wizara hiyo ya afya imetenga jumla ya shilingi bilioni 270, tofauti na mwaka wa fedha (2015-16) ambapo zilikuwa milioni 30 hivyo hawatarajii kusikia sehemu za kutolewa huduma zake za kiafya kuwa zina upungufu wa dawa.
Akiwa katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga na Kituo cha Afya cha Kambarage manispaa ya Shinyanga na kukagua bohari za dawa, Dk. Ndugulile alitoa tahadhari kwa wauguzi kuwa ni marufuku dawa hizo za serikali kukutwa zinauzwa kwenye maduka ya watu binafsi na ikibainika watachukuliwa hatua kali.
“Serikali ya awamu hii ya tano imedhamiria kuboresha huduma za afya hapa nchini, na ndio maana hata bajeti yake imetolewa ni ya fedha nyingi hivyo sisi kama wizara husika hatutarajii kuwepo kwa upungufu wa dawa kwenye sehemu za huduma za afya”,alieleza.
Pia aliwataka wananchi kujiunga na Bima ya afya ya jamii CHF iliyoboreshwa, ili kuwa na uhakika wa kupata matibabu hasa pale watakapougua na kukutwa hawana pesa ambapo wataweza kutibiwa kwa shilingi hiyo 10,000/=  ili kuokoa maisha yao.
Naye kiongozi wa Mradi wa Maendeleo ya Tuimarishe Afya (HPSS) kutoka makao makuu Dodoma Profesa Manoris Meshack, alisema mradi huo wa Bima ya afya ya jamii CHF ulianza mwaka 2011 mkoani Dodoma, na baada ya kufanya vizuri mwaka 2015 ukaongezwa katika mikoa miwili ya Shinyanga na Morogoro.
Alitaja takwimu za kaya katika mikoa hiyo mitatu zilizojiunga na CHF iliyoboreshwa hadi sasa kuwa ni 318,334 sawa na asilimia 26 kati ya kaya 1,220,413, na hadi kufikia Disemba 2017 kupitia uandikishaji wa wanachma wamekusanya shilingi bilioni 7,027,605,547. ambapo shilingi bilioni 2,435,194,000 ni malipo ya tele tele.
Nao baadhi ya wazee kati ya kumi wasiojiweza ambao walikatiwa Bima hiyo ya Afya ya jamii CHF iliyoboreshwa na Naibu Waziri huyo wakati wa ziara hiyo,Mohamed Mkumbola na Regina Kulwa waliipongeza serikali kwa kujali makundi hayo maalumu, na kuomba wazee wote wakatiwe Bima hiyo pamoja na kuendelea kutoa elimu kwa wananchi wajiunge.
ANGALIA PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA ZIARA
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwa katika bohari ya dawa kwenye kituo cha afya kata ya Kambarage mjini Shinyanga. Picha zote na Marco Maduhu na Steve Kanyefu
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwa ameshika kopo la dawa katika bohari ya dawa kwenye kituo cha afya Kambarage mjini Shinyanga na kusisitiza kuwa dawa zenye nembo ya dawa za serikali MSD hazitakiwi kutoka nje ya hospitali za serikali.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akimsalimia mgonjwa katika kituo cha Afya Kambarage mjini Shinyanga huku akiangalia dawa alizopewa mgonjwa na kupiga marufuku wagonjwa kuambiwa dawa hakuna na kwenda kununua kwenye maduka ya dawa ya watu binafsi.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulileakikagua chumba cha upasuaji katika kituo cha afya Kambarage mjini Shinyanga, na kuagiza jengo hilo lifanyiwe marekebisho ili kuendana na hadhi ya chumba cha upasuaji, sababu haliridhishi kuendana na huduma ambayo itakuwa ikitolewa.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akitoka kwenye jengo la chumba cha upasuaji katika kituo cha afya kata ya Kambarage mjini Shinyanga na kuacha maagizo lifanywe marekebisho.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akihamasisha wananchi wa kata ya Kambarage mjini Shinyanga kujiunga na Bima ya afya ya jamii CHF iliyoboreshwa, ili kuwa na uhakika wa kupata matibabu pale watakapo patwa na ugonjwa gafla harafu hawana pesa ambapo bima hiyo itasaidia kupata tiba na kuokoa maisha yao.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akitoa hamasa kwa wananchi kwa vitendo juu ya ukataji wa Bima ya afya ya jamii CHF iliyoboreshwa, na kukata Bima hiyo papo hapo, na hapo akipigwa picha na Ofisa uandikishaji CHF Kata hiyo ya Kambarage Marry Budigila.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akijaza taarifa zake wakati akiendelea na zoezi la ukataji Bima hiyo ya afya ya jamii CHF iliyoboreshwa, na kutoa hamasa kwa wanachi kujiunga nayo huku akikatia watu 10 bima hiyo ambao hawajiwezi wakiwamo wazee.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akitoa hamasa ya wananchi kujiunga na bima hiyo ya Afya CHF iliyoboreshwa, pamoja na kusaidia kuwaunga watu watano wasiojiweza kwenye Bima hiyo.Matiro alimuunga mkono Naibu waziri kwa kutoa elimu kwa vitendo huku akiwataka wadau kujitokeza kusaidia kukatia Bima hiyo watu waliokatika makundi maalumu.
Ofisa uandikishaji wa Bima ya afya CHF iliyoboreshwa Jackson Njau, akiendelea na zoezi la kuingiza taarifa kwa wananchi ambao wamejitokeza kujiunga na Bima hiyo ya afya ya jamii.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akimkabidhi Kadi ya CHF Mzee Mohamed Mkumbola ambaye ni miongoni mwa watu 10 wasiojiweza aliowakatia Bima hiyo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akimkabidhi kadi ya CHF bi Regina Kulwa ambaye ni miongoni mwa watu 10 wasiojiweza aliowakatia Bima hiyo.
Mzee Mohamed Mkumbola akitoa shukrani kwa Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile kwa kuwakatia kadi ya bima ya afya wazee wasiojiweza, huku akimuomba kumsaidia kupata madai yake katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga anayodai mara baada ya kuacha kufanya kazi, ombi ambalo liliahidiwa kushughulikiwa na kukabidhiwa majukumu hayo katibu Tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela.
Baadhi ya wananchi wa kata ya Kambarage mjini Shinyanga, wakisikiliza nasaha kutoka kwa Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile juu ya kujiunga na Bima hiyo ya afya CHF, ambayo itakuwa msaada mkubwa katika kuokoa maisha yao pale watakapopatwa na magonjwa na kukutwa hawana pesa.
Baadhi ya wananchi wa kata ya Kambarage mjini Shinyanga wakiwa kwenye mkutano wa hamasa ya kujiunga na Bima ya CHF iliyoboreshwa, ambapo mtu akikata shilingi 10,000 yeye na familia yake watu watano watatibiwa bure kwa mwaka mzima.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwa katika hospitali ya Rufaa mkoani Shinyanga kuangalia namna huduma za afya zinavyotolewa dhidi ya wananchi, huku upande wa mkono wa kushoto ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro, na mkono wa kulia ni mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Dk. Geogre Masigati.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiangalia huduma ya mfumo wa malipo ya kielekroniki kwenye hospitali hiyo ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga, na kukuta mfumo huo haufanyi kazi ambapo hapo awali aliambiwa unafanya kazi na kusababisha kuwepo na upotevu wa fedha.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiangalia majalada ya wagonjwa na namna wanavyopatiwa huduma za matibabu katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akimsalimia mzazi katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga, na kumuliza maswali juu ya huduma anazopewa ikiwemo kama aliagizwa kwenda kununua dawa yoyote ama vifaa kwa ajili ya kujifunguli na kupewa majibu kuwa kahudumiwa vizuri na vitu vyote kapewa hapo hospitalini.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akipitia taarifa ya hospitali hiyo ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga na kubaini kuna upotevu mkubwa wa pesa kutokana na kutofanya kazi mfumo wa ukusanyaji pesa kwa njia ya kielektroniki na kuagiza ufanye kazi haraka sana.
Baadhi ya wauguzi katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga wakisikiliza ujumbe kutoka kwa Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile na kusisitizwa watoe tiba vizuri kwa wananchi pamoja na kutoa kauli nzuri kwa wagonjwa.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro, akimkaribisha Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile kusikiliza taarifa za huduma ya afya kutoka kwa wakurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga na Shinyanga vijijini
Mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga Geofrey Mwangulumbi akisoma taarifa ya huduma ya afya ya manispaa hiyo. Alisema katika manispaa hiyo kuna vituo Viwili vya afya, zahanati 28 na hakuna tatizo la uhaba wa dawa,na kutaja takwimu za Kaya zilizojiunga na bima ya afya ya jimii CHF kuwa ni Kaya 7,136 sawa na asilimia 21.2 ya kaya zote, na kaya zilizo hai hadi sasa ni 3,781na zinaendelea kupata huduma ya matibabu sawa na asilimia 11.2, ambapo lengo la kitaifa ni kufikia asilimia 30 na kuwataka wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi kujiunga na bima hiyo ya CHF.
Mkurugenzi wa halmashuari ya Shinyanga vijijini Bakari Kasinyo, akisoma taarifa ya huduma za afya kwenye halmshauri hiyo ambapo alisema kuna vituo vya afya vitano na zahanati 35 na hakuna tatizo la dawa na kutaja idadi ya kaya zilizojiunga na bima ya CHF iliyoboreshwa,kuwa ni 10,615 kati ya kaya 59,321 sawa na asilimia 11.3 ,na kubainisha mkakati ulipo ni kuendelea kutoa hamasa kwa wananchi kujiunga na Bima hiyo ya CHF.
Kiongozi wa mradi wa maendeleo ya tuimarishe afya (HPSS) kutoka makao mkuu Dodoma Prof Manoris Meshack, akisoma taarifa ya mradi huo wa Bima ya afya ya jamii CHF kuwa ulianza mwaka 2011 mkoani Dodoma, na baada ya kufanya vizuri mwaka 2015 ukaongezwa katika mikoa miwili ya Shinyanga na Morogoro.
Alitaja takwimu za kaya katika mikoa hiyo mitatu zilizojiunga na CHF iliyoboreshwa hadi sasa kuwa ni 318,334 sawa na asilimia 26 kati ya Kaya 1,220,413 na hadi kufikia Dicemba 2017 kupitia uandikishaji wa wanachma wamekusanya shilingi bilioni 7,027,605,547. ambapo shilingi bilioni 2,435,194,000 ni malipo ya tele tele.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwa na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro wakikagua Jengo la Hospitali mpya ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga ambayo inajengwa katika kata ya Mwawaza manispaa ya Shinyanga.
Muonekano wa nje wa jengo jipya la hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga.
Picha zote na Marco Maduhu na Steve Kanyefu

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa