Home » » MADIWANI WAACHIA NGAZI CHADEMA

MADIWANI WAACHIA NGAZI CHADEMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Madiwani wa wili wa chama cha chadema katika manspaa ya Shinyanga wameachia nafasi zao kwa madai ya kukosa imani na uongozi wa juu wa chama hicho kwa kuendekeza migogoro na kuwaita baadhi ya wanachama wasaliti.
Madiwani waliongatuka katika chama hicho ni Sebastian Peter diwani wa kata ya Ngokolo na Zacharia mfuko kata ya Masekolo ambao wamekabidhi barua zao kwa mkurugenzi wa manspaa ya Shinyanga.
Awali wakiongea na waandishi wa habari madiwani hao wanasema  uongozi wa juu wa chama hicho umekuwa ukiendekeza migogoro ndani ya chama pamoja na ubinafisi pia ahadi zao zimekuwa sio za kweli za kumjengea nyumba mjana wa aliyekuwa mgombea ubunge marehemu Shilembi magadula.
Aidha madiwani hao wamesema migogoro hiyo itasababisha kukisambaratisha chama hichi kwani viongozi wa juu akiwemo katibu mkuu na mwenyekiti wamekuwa na ubaguzi wa ukabira
Katibu wa chama cha chadema mkoa wa Shinyanga Nyangaki Shilungu Shella amesema chama chake kimepata pigi lakini watajipanga vyema kuhakikisha kata hizo wanazichukuwa wakati wa uchaguzi mdogo.
Chadema walikuwa na madiwani 8 baada ya 2 kuachia ngazi wamebaki 6 wakati ccm wakiwa na madiwani 17 katika baraza la madiwani.
 

0 comments:

 
Supported by Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa