Home » » LIKIZO YA MALIPO NI HAKI YA MWAJIRIWA

LIKIZO YA MALIPO NI HAKI YA MWAJIRIWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Lumato anasema hata eneo likionyesha dalili nzuri za awali kama ilivyo katika Bonde la Ruhuhu ni lazima sehemu hiyo ichimbwe na matokeo yaonyeshe kiasi cha rasilimali kinachoweza kuzalishwa kibiashara

Makala hii inamsaidia mwajiri na mwajiriwa kujua jinsi ya kupeana na kuomba likizo kwa mujibu wa sheria ya ajira na mahusiano kazini na. 6 ya mwaka 2004. Sheria hii inatoa muongozo jinsi ya kupeana likizo na aina ya likizo ambazo muajiriwa anapaswa kupewa.
Likizo zote anayepaswa kupewa ni yule aliyefanya kazi zaidi ya miezi sita mfululizo, au kama alifanya akatoka halafu akafanya tena basi hizo siku zisizidi miezi sita atakuwa na haki ya kupata likizo. Tunapoongelea likizo tuna maana likizo yenye malipo, siyo unampa mtu likizo lakini mshahara haumpi hicho ni kinyume cha sheria.
Likizo ya mwaka (Annual Leave) hii ni likizo ya siku 28 ambayo kila mfanyakazi anapaswa kuipata kila mwaka, haijalishi mfanyakazi huyu yuko sekta gani iwe mlinzi, dereva au mfanyakazi wa ndani.
Hii likizo inapaswa kutolewa na mwajiri na endapo mtakubaliana kuwa badala ya kwenda likizo mfanyakazi huyu anapaswa kuendelea kufanyakazi basi mshahara wa mwezi mmoja alipwe huyu mfanyakazi kwa mujibu wa kifungu cha 31 cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya mwaka 2004.
Likizo ya ugonjwa (Sick Leave), hii ni likizo inayotolewa kwa mgonjwa ambaye ni mwajiriwa na ana haki ya kupata likizo hii ya ugonjwa ambayo ni siku 126, siku 63 ni mshahara wote na siku 63 zinazofuata nusu mshahara, pia mtu huyu hawezi kupewa likizo hii endapo atashindwa kutoa uthibitisho wa daktari au endapo anapewa mafao kutoka kwenye makubaliano ya pamoja au kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii.
Likizo ya kifo (Compassionate Leave), hii ni likizo kwa mfiwa, endapo mfanyakazi atafiwa na mtu wake wa karibu, baba, mama, dada, mke au mtoto ana haki ya kupata likizo ya siku nne. Pia likizo hii inaruhusiwa endapo mfanyakazi anauguliwa na mtoto mdogo.
Hii ni haki ya mfanyakazi endapo atathibitisha uwepo wa hilo tukio tajwa, hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 34 cha Sheria ya Ajira ya mwaka 2004.
Likizo ya Uzazi kwa mwanamke (Maternity Leave) ni likizo maalumu ya siku 84 na endapo atajifungua watoto mapacha basi anapata likizo ya siku 100, pia huyu mwajiriwa anapaswa kupewa muda wa saa mbili wa kazi kwa ajili ya kumnyonyesha mtoto, endapo mtoto atafariki ndani ya mwaka mmoja anapaswa kupewa likizo ya uzazi endapo atashika mimba.
Taarifa ya likizo itolewe kwa mwajiri ndani ya miezi mitatu juu ya lini likizo inachukuliwa. Pia mama anayenyonyesha haruhusiwi kufanya kazi zinazohatarisha afya yake na ya mtoto, mjamzito anaweza kuchukua wakati wowote wiki nne kabla ya kujifungua na inawezakuwa mapema zaidi endapo daktari atathibitisha hilo.
Likizo ya uzazi kwa mwanaume (Paternity Leave) hii ni likizo maalumu kwa wanaume ambao wake zao wamejifungua.
Ni likizo ya siku tatu na inapaswa kuchukulia ndani ya siku saba toka mke kajifungua, unachopaswa ni kumtaarifu mwajiri na kuthibitisha kuwa aliyejifungua ni mkeo, hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 34 (1) a cha sheria ya ajira ya mwaka 2004. Kimsingi ni suala la msingi sana kwa wafanyakazi kuzijua haki zao.
Makala hii itaendelea alhamisi ijayo, waambie waajiriwa wengine waisome ili waweze kujua haki zao ambazo nyingi zinamezwa na baadhi ya waajiri nchini
 Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa