Home » » MWILI WA MUFTI KUSAFIRISHWA KESHO MKOANI SHINYANGA

MWILI WA MUFTI KUSAFIRISHWA KESHO MKOANI SHINYANGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


ufti ,Alhaj Sheikh Shaban Issa Bin Simba enzi za uhai wake.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
MWILI wa  Mufti ,Alhaj Sheikh Shaban Issa Bin Simba unatarajiwa kusafirishwa kesho mkoani Shinyanga.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Makao Makuu ya Baraza Kuu la Waislam Tanzania (Bakwata),Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam,Alhaj Alhad Mussa Salum amesema mwili wa marehemu utaswaliwa kesho katika Msikiti wa Msilimu ,viongozi mbalimbali wa dini na serikali watakuwepo.

Amesema marehem alikuwa akisumbuliwa na sukari,Shinikizo la Damu (BP)  pamoja na Figo.
Hata hivyo amesema kuwa jana (Jumapili) Mufti alifanyiwa oparesheni ya figo katika Hospitali ya TM Jijini Dar es Salaam na Mauti ya Mufti yamekuta majira ya saa moja leo.

Salum amesema marehem anatarajiwa kuzikwa Alhamis mkoani mkoani Shinyanga 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa