Jumamosi
 Februari 18,2017,kumefanyika kikao cha kamati ya Maandalizi ya Mkutano 
Mkuu na sherehe za kumuaga Askofu wa Kanisa la African Inland Church 
Tanzania (AICT) Dayosisi ya Shinyanga Dkt.John Kanoni Nkola ambaye 
anastaafu uaskofu mwezi Agosti mwaka 2017. 
Kikao 
hicho kilichofanyika katika ukumbi wa NSSF mjini Shinyanga ambapo mamia 
ya wachungaji,viongozi na waumini wa kanisa hilo dayosisi ya Shinyanga 
ambapo mgeni rasmi alikuwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mheshimiwa 
Josephine Matiro. 
Mnenaji
 mkuu katika kikao hicho alikuwa Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi 
Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala. 
Akizungumza
 wakati wa kikao hicho Askofu Dkt. Makala aliwapongeza viongozi wa 
kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga wakiongozwa na Katibu mkuu wa 
kanisa hilo,Mchungaji Jakobo Mapambano kwa kuandaa sherehe ya kumuaga 
Askofu Nkola ambaye amekuwa askofu wa Kanisa hilo tangu tarehe 
24.10.1993. 
Askofu
 Makala alitumia fursa hiyo kuwaonya waumini wa kanisa hilo kutokuwa na 
tamaa ya madaraka ya uongozi kwa nafasi itakayoachwa na Askofu Nkola 
hili kuepuka vurugu zinazoweza kujitokeza na kusisitiza kuwa ni vyema 
kiongozi atakayeziba nafasi hiyo apatikane kwa utaratibu unaotakiwa.
Akizungumza
 wakati wa kufungua kikao hicho,mgeni rasmi,Mkuu wa wilaya ya Shinyanga 
Josephine Matiro alitumia fursa hiyo kuwakumbusha viongozi wa dini 
kuongeza nguvu katika kueneza neno la mungu kwani watu wengi katika mkoa
 wa Shinyanga bado hawajamjua vyema mungu,wengi wao hawana dini.
Katika
 hatua nyingine Matiro aliwaomba viongozi wa dini kuiunga mkono serikali
 katika vita dhidi ya dawa za kulevya kwa kuhubiri watu waachane na 
vitendo.Mwandishi
 mkuu wa Malunde1 blog,Kadama Malunde,alikuwepo katika kikao 
hicho…Ametuletea picha 50 za matukio yaliyojiri katika kikao 
hicho…Tazama hapa chini.
Mkuu 
wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiwasalimia viongozi wa kanisa 
la AICT Dayosisi ya Shinyanga wakati akiwasili katika ukumbi wa NSSF 
mjini Shinyanga kuhudhuria kikao chakikao cha kamati ya Maandalizi ya 
Mkutano Mkuu na sherehe za kumuaga Askofu wa Kanisa la African Inland 
Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Shinyanga Dkt. John Kanoni Nkola 
ambaye anastaafu uaskofu mwezi Agosti mwaka 2017 .Kulia ni Makamu wa 
Askofu Dayosisi ya Shinyanga mchungaji Aaron Malyuta
Mkuu 
wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiwasalimia viongozi wa kanisa 
la AICT Dayosisi ya Shinyanga akisalimiana na wachungaji wa kanisa la 
AICT
Ndani 
ya ukumbi wa NSSF: Kushoto ni Katibu mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya 
Shinyanga,Mchungaji Jakobo Mapambano,katikati ni mkuu wa wilaya ya 
Shinyanga ,Josephine Matiro na Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini 
Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala baada ya kuwasili
 ukumbini.
Maombi yakiendelea baada ya mgeni rasmi kuwasili ukumbini
Wajumbe wa kikao hicho wakisali ukumbini
Katibu
 mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Jakobo Mapambano
 akitambulisha viongozi na wageni mbalimbali waliohudhuria kikao hicho Askofu
 wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga, Dr. John Nkola.Hakuwepo wakati
 wa Kikao cha leo(Picha kutoka Maktaba ya Malunde1 blog
Askofu
 wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga, Dr. John Nkola.Hakuwepo wakati
 wa Kikao cha leo(Picha kutoka Maktaba ya Malunde1 blog
Katibu
 mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Jakobo Mapambano
 alisema kikao hicho ni hatua ya awali ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu na 
sherehe za kumuaga Askofu wa Kanisa la African Inland Church Tanzania 
(AICT) Dayosisi ya Shinyanga Dkt.John Kanoni Nkola ambaye anastaafu 
uaskofu mwezi Agosti mwaka 2017.
mkuu 
wa wilaya ya Shinyanga ,Josephine Matiro na Askofu wa Kanisa la KKKT 
Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala 
wakimsikiliza mchungaji Mapambano
Katibu
 mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Jakobo Mapambano
 akiwapungia mkono wajumbe wa kikao hicho kutoka ndani na nje ya mkoa wa
 Shinyanga
Makamu
 wa Askofu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Aaron 
Malyuta akizungumza wakati wa kuthibitisha tamko la kuwakaribisha 
wajumbe na wageni katika kikao hicho
Wajumbe wakiwa ukumbini
Kwaya AICT Shinyanga wakiimba ukumbini
Kwaya ya AICT Shinyanga ikiimba
Wajumbe wakiwa ukumbini
wajumbe wa kikao hicho wakiwa wamesimama
Makamu wa Askofu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Aaron Malyuta akizungumza ukumbini
Kikao kinaendelea
Wajumbe wakiwa ukumbini
Kikao kinaendelea
Mwenyekiti
 wa kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu na sherehe za kumuaga Askofu wa
 Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Shinyanga 
Dkt.John Kanoni Nkola,Erasto Kwilasa ambapo aliwaomba viongozi na 
waumini wa kanisa hilo kushirikiana naye katika kufanikisha mkutano huo 
na sherehe hizo
Kwaya AICT Kambarage ikiimba
Viongozi
 wa kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu na sherehe za kumuaga Askofu wa
 Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Shinyanga 
Dkt.John Kanoni Nkola wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini
Kushoto
 ni Katibu mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Jakobo
 Mapambano na mkuu wa wilaya ya Shinyanga ,Josephine Matiro wakiwa 
wamesimama ukumbini
Viongozi wa Kanisa wakiwa ukumbini
Maombi yakiendelea kabla ya Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala
Maombi yanaendelea
Askofu
 wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. 
Emmanuel Joseph Makala akizungumza wakati wa kikao hicho ambapo 
aliwataka waumini kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga kuyaenzi mambo 
mazuri yote yaliyofanywa na Askofu Dkt. John Nkola
Askofu
 wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. 
Emmanuel Joseph Makala pia aliwahamasisha waumini wa kanisa hilo 
kudumisha upendo
Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala akizungumza ukumbini
Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala akiendelea kuzungumza
Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala akitoa neno ukumbini
Askofu
 wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt. 
Emmanuel Joseph Makala akiwa amesimama baada ya kumaliza kuzungumza
Meza kuu wakiwa wamesimama,wa kwanza kushoto ni mchungaji Samwel Njile kutoka Kanisa la AICT Pastoreti ya Masumbwe mkoani Geita
Kikao kinaendelea
Wajumbe wa kikao wakiwa ukumbini
Maombi yanaendelea
Makamu wa Askofu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Aaron Malyuta akizungumza ukumbini
Mchungaji
 Samwel Njile kutoka Kanisa la AICT Pastoreti ya Masumbwe mkoani Geita 
akiteta jambo na Katibu mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya 
Shinyanga,Mchungaji Jakobo Mapambano
Wajumbe wa kikao 
Makamu
 wa Askofu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Aaron 
Malyuta akimkaribisha mgeni rasmi,mkuu wa wilaya ya Shinyanga ili 
azungumze na wajumbe wa kikao hicho
Mkuu 
wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza ukumbini ambapo 
aliwapongeza waumini wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga kuandaa 
sherehe maalum kumuaga Askofu Dkt. Nkola
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza ukumbini
Mkuu 
wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akisisitiza umuhimu wa kufikisha
 neno la mungu katika maeneo mengi zaidi ili wananchi wawe na hofu ya 
mungu
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza katika kikao hicho
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akisisitiza jambo
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiendelea kuzungumza
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akishikana mkono na mchungaji Mapambano baada ya kumaliza kuzungumza
Kushoto
 ni Katibu mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Jakobo
 Mapambano,katikati ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ,Josephine Matiro na 
Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Dkt.
 Emmanuel Joseph Makala wakiwa ukumbini
Katibu
 mkuu wa kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga,Mchungaji Jakobo Mapambano
 akimsindikiza Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya 
Ziwa Victoria,Dkt. Emmanuel Joseph Makala kutoka ukumbini baada ya kikao
 hicho kufunguliwa na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.
Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment