Home » » MKUU WA SHULE KAHAMA B KULA SAHANI MOJA NA WAZAZI BAADA YA SIKU TATU.

MKUU WA SHULE KAHAMA B KULA SAHANI MOJA NA WAZAZI BAADA YA SIKU TATU.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.


Uongozi wa Shule ya Msingi Kahama(B), iliyopo Halmashauri ya Mji wa Kahama, umesema baada ya siku tatu, utachukua hatua  za kinidhamu kwa wanafunzi watoro   ambao  wameshindwa kuhudhuria masomo, licha ya  muhula wa kwanza wa masomo kuanza leo.

Akizungumza na Kijukuu Blog, Mwalimu Mkuu wa Shule  hiyo, CONRAD NKUBA amesema licha ya shule kufunguliwa, bado kuna baadhi ya wanafunzi wameshindwa kuhudhuria masomo.

NKUBA amewataka wazazi na walezi kuwahimiza wanafunzi kuhudhuria masomo na si kukaa nao na kuwatumikisha shughuli za nyumbani.

Naye Mwalimu wa Taaluma katika shule ya Msingi Majengo,  LETICIA  BUCHUMA amesema katika shule hiyo mahudhurio  ya wanafunzi kwa siku ya kwanza, ni mazuri ingawa bado kuna baadhi ya wanafunzi ni watoro.

Muhula wa Kwanza wa Masomo katika shule za Msingi na Sekondari nchini, umeanza  baada ya shule kufunguliwa rasmi  leo Januari 8.
Kijukuu

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa