Home » » HALMASHAURI ZATAKIWA KUTOA RUZUKU KWA SHULE BINAFSI

HALMASHAURI ZATAKIWA KUTOA RUZUKU KWA SHULE BINAFSI

Mwandishi wetu, Kahama-Shinyanga Yetu
HALMASHAURI za wilaya, miji, Manispaa na Majiji zimetakiwa kutenga bajeti ya kusaidia shule binafsi kwa kuwa mchango zinazotoa katika Taifa ni sawa na zile za Serikali ambazo zinapata misaada mingi kutoka serikalini.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mhongolo iliyopo wilayani Kahama Jeremiah Gunda wakati akitoa taarifa fupi kwenye mahafari ya saba ya Shule hiyo.
Katika mahafari hayo Mwalimu gunda alisema shule hizo binafsi zinazalisha watoto wengi kwenda kupata elimu za juu lakini Serikali haizishirikishi ikiwemo walimu wake kuwapeleka kwenye semina mbalimbali zitolewazo kupitia Halmashauri hizo.
Hata hivyo Afisa Elimu Taaluma katika Halmashauri ya mji wa Kahama;bi Annastazia Manumbu alisema hali hiyo inawezekana kwakuwa mchango mkubwa utolewao na shule hizo kitaaluma huonekana katika jamii hivyo alisema atalifikisha  kwenye     vikao husika .
Manumbu amewataka wazazi wasibweteke na elimu waliyoipata watoto wao hivyo wakati wa kusubiri matokeo ya mitihani yao ni bora wakawapeleka kujiendeleza na masomo mengine kuliko kuwaacha wakizagaa mitaani
Blogzamikoa

0 comments:

 
Supported by Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa