Home » » MADEREVA ‘BODABODA’ 700 WAPEWA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI KAHAMA

MADEREVA ‘BODABODA’ 700 WAPEWA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI KAHAMA

Mwandishi wetu, Kahama-Shinyanga Yetu
ZAIDI ya bodaboda mia saba wanaofanya biashara ya kusafirisha abiria kwa kutumia pikipiki wilayani Kahama wamepatiwa mafunzo ya usalama barabarani hali itakayopunguza vifo vitokanavyo na ajali.
Mkuu wa Usalama barabarani wilayani Kahama Mkaguzi Msaidizi bwana Robert Siwendo amesema mafunzo hayo yamedhaminiwa na benki ya CRDB Tawi la Kahama na kuwashirikisha vijana hao wa Bodaboda.
Aidha bwana Siwendo amesema mafunzo hayo yamekuja baada ya idadi kubwa ya vijana hao kubainika wanafanya shughul hizo bila kufuata misingi ya Sheria ya usalama barabarani ikiwemo kuendesha pikipiki bila kuvaaa kofia nzito pamoja na wengine kutokuwa na reseni.
Amesema mbali na hayo pia pikipiki hizo zimekuwa zikikodiwa na Waharifu hali ambayo imekuwa ikihatarisha maisha yao kwa kuuawa na kunyang’anywa mali zao ikiwa sababu kubwa ni vijana hao kutokuwa makini wakati wa kazi zao.
Kwa upande wake Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Kahama iliyodhamini mafunzo hayo bwana Said Pamuye amesema utaratibu huu utakuwa endelevu kwani kuwapa mafunzo hayo watakuwa na uwezo wa kufahamu sheria za Usalama barabarani hali itakayopunguza matatizo wanayokumbana nayo wakiwa kazini.
Blogzamikoa

0 comments:

 
Supported by Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa