Home » » Anusurika kifo baada ya kuchinjwa na baba yake

Anusurika kifo baada ya kuchinjwa na baba yake

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MWANAFUNZI wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Majengo wilayani Kahama, Shinyanga, Said Siraji (13), amenusurika kufa baada ya kuchinjwa shingo na baba yake mzazi.
Hivi sasa mtoto huyo amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama ambapo Mganga Mkuu wa hospitali hiyo Dk. Joseph Fwoma alikiri kumpokea mwanafunzi huyo jana alfajiri baada ya kuokolewa na raia wema wakati akikimbia huku akivuja damu shingoni.
Dk. Fwoma alisema alipofika hospitalini hapo madaktari walimfanyia upasuaji na kumshona sehemu ya koromeo lililochinjwa huku akibainisha kwamba hali yake inaendelea vizuri baada ya kuongezwa damu.
 Chanzo;Tanznia Daima

0 comments:

 
Supported by Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa