Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Wengi tumekuwana tukizifahamu aina mbalimbali za njugu kama vile karanga,korosho na nazi.
Lozi ni moja wapo ya njugu ambazo jina lake 
maarufu duniani ni Almonds. Yenyewe hukaangwa kidogo na huliwa kwa 
kutafunwa kama ilivyo karanga.
Kitafunwa hiki kinachofanana na karanga kinatajwa 
kuwa ni tiba kwa watu wenye matatizo ya moyo na husaidia kwa kiasi 
kikubwa katika kuratibu mapigo ya moyo.
Pamoja na hilo utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu 
cha Purdue unaonyesha lozi kuwa na manufaa mengi kiafya ukilinganisha na
 aina nyingine za njugu.
Hiyo inatokana na kiwango kikubwa cha protini na 
virutubisho vingine kama vile madini na kusaidia kuratibu mfumo mzima wa
 mwili, moja wapo maradhi ya moyo.
Mtafiti katika Bodi ya Sayansi Jimbo la California
 nchini Marekani, Dk Karen Lapsley ambaye ni mmoja wa wataalam 
walioshiriki katika utafiti huo anasema lozi pia inasadia kwa kiasi 
kikubwa kupunguza kasi ya ugonjwa wa kisukari.
Anasema kuwa mtu mwenye kisukari anapotafuna lozi 
zinamsaidia kuratibu mfumo wake damu na kuhakikisha siku zote mishipa ya
 damu inakuwa inafanya kazi inavyostahili.
  Dk Penny Kris Etherton wa chuo kikuu cha 
Pennsylvania anasema lozi zina uwezo mkubwa wa kupunguza kiwango cha 
lehemu ndani ya mwili.
Madini yaliyomo kwenye lozi yanasaidia kuimarisha 
mifupa, misuli, viungo na kukabiliana na shinikizo la damu. Matatizo 
haya mara nyingi hujitokeza kjwa wenye umri mkubwa.
Chanzo:Mwananchi
Chanzo:Mwananchi
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment