Home » » LOZI;AINA YA NJUGU YENYE MANUFAA MENGI MWILINI

LOZI;AINA YA NJUGU YENYE MANUFAA MENGI MWILINI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Wengi tumekuwana tukizifahamu aina mbalimbali za njugu kama vile karanga,korosho na nazi.
Lozi ni moja wapo ya njugu ambazo jina lake maarufu duniani ni Almonds. Yenyewe hukaangwa kidogo na huliwa kwa kutafunwa kama ilivyo karanga.
Kitafunwa hiki kinachofanana na karanga kinatajwa kuwa ni tiba kwa watu wenye matatizo ya moyo na husaidia kwa kiasi kikubwa katika kuratibu mapigo ya moyo.
Pamoja na hilo utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Purdue unaonyesha lozi kuwa na manufaa mengi kiafya ukilinganisha na aina nyingine za njugu.
Hiyo inatokana na kiwango kikubwa cha protini na virutubisho vingine kama vile madini na kusaidia kuratibu mfumo mzima wa mwili, moja wapo maradhi ya moyo.
Mtafiti katika Bodi ya Sayansi Jimbo la California nchini Marekani, Dk Karen Lapsley ambaye ni mmoja wa wataalam walioshiriki katika utafiti huo anasema lozi pia inasadia kwa kiasi kikubwa kupunguza kasi ya ugonjwa wa kisukari.
Anasema kuwa mtu mwenye kisukari anapotafuna lozi zinamsaidia kuratibu mfumo wake damu na kuhakikisha siku zote mishipa ya damu inakuwa inafanya kazi inavyostahili.
  Dk Penny Kris Etherton wa chuo kikuu cha Pennsylvania anasema lozi zina uwezo mkubwa wa kupunguza kiwango cha lehemu ndani ya mwili.
Madini yaliyomo kwenye lozi yanasaidia kuimarisha mifupa, misuli, viungo na kukabiliana na shinikizo la damu. Matatizo haya mara nyingi hujitokeza kjwa wenye umri mkubwa.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa