Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willbrod Slaa
Vyama hivyo vya Chadema, NCCR-Mageuzi na CUF, viongozi wake wandamazi nje ya Bunge walianza ziara ya kutembelea mikoani kuwaelimisha wananchi umuhimu wa katiba
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya NCC-Mageuzi, Hemed Msabaha, akizunguma katika mkutano wa hadhara w uliofanyika mjini Geita, juzi alisema umoja wao umejipanga kupambana na CCM katika uchaguzi mkuu wa 2015.
Msabaha alisema wamepeana majukumu ambayo Chadema kitakuwa kinafanya mashambulizi ya angani kwa kufanya ziara
mikoani kwa kutumia helkopita nchi nzima.
Alisema CUF kinachoongozwa na Mwenyekiti wake,Profesa Ibrahimu Lipumba, kimepewa jukumu la kufanya mashambulizi ya
nchi kavu ili kuhakikisha CCM haifanyi hila zozote za kuhujumu uchaguzi huo.
Msabaha alisema NCCR-Mageuzi kinaongozwa na James Mbatia, kitaendesha mashambulizi majini lengo likiwa ni kuhakikisha kura haziibiwi mwakani.
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willbrod Slaa, aliwataka wananchi kuwaunga mkono katika harakati za kupata katiba bora na
kupinga hujuma alizodai zinataka kufanywa na CCM kuhujumu katiba mpya.
Dk. Slaa alisema umoja wao utaendelea hadi u2015 na kusisitiza kuwa kama CCM itang’ang’ania suala la muundo wa serikali tatu lisijadiliwe katika Bunge Maalum la Katiba, wabunge wa Ukawa hawatakuwa tayari kurejea katika bunge hilo.
SOURCE:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment