Home » » TAASISI ZA FEDHA NCHINI ZATAKIWAKUTOA MIKOPO KWA WALEMAVU

TAASISI ZA FEDHA NCHINI ZATAKIWAKUTOA MIKOPO KWA WALEMAVU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

SHIRIKISHO la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu Wilayani Kahama, mkoani Shinyanga (SHIVYAWATA)wamezitaka taasisi za fedha zinazotoa mikopo ya ujasiriamali kuwakopesha baadhi ya wanaohitaji kuchukua mkopo badala ya kuwaona kama hawawezi na kuwabagua.

Wakizungumza juzi katika mkutano wa tathmini na ufuatiliaji kuhusu utekelezaji wa sheria ya watu wenye ulemavu namba 9 ya mwaka 2010 uliofanyika ofisini kwao mjini Kahama wamezitaka taasisi za fedha zinazotoa mikopo ya ujasiriamali kuwakopesha kama watu wengine bila ubaguzi.

Bi.Kuruthumu Jafari alisema baadhi ya watu wenye ulemavu wamekuwa wakijishughulisha na ujasiriamali mbalimbali, lakini tatizo kubwa wamekuwa wakihitaji msaada wa kuwezeshwa kukopeshwa waweze kuwa na ufanisi wa kazi yao.

Mwenyekiti wa SHIVYAWATA wa wilaya ya Kahama, Bw.Marco Kanjiwa alisema watu wenye ulemavu ni sawasawa na mtu yeyote katika kazi za ujasiriamali na kuzitaka taasisi za fedha zinazotoa mkopo ziweze kuwakopesha wanapohitaji.

Akizungumzia kuhusu sheria namba 9 ya mwaka 2010 inayohusu watu wenye ulemavu iliyotungwa na bunge Kanjiwa alisema jamii bado haijawa na uelewa kuhusu sheria hiyo na kuwataka maofisa maendeleo ya jamii kuwaelimisha wananchi na kuisimamia popote kazini kwao.

Makamu Mwenyekiti wa SHIVYAWATA wa wilaya ya Kahama Bw.Sitta Masenya alizitaka mamlaka zote za serikali kuendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya sheria ya watu wenye ulemavu kwa sababu bado miongoni mwa baadhi ya jamii kuna tatizo la kuwaficha huku wengine wakiendelea kuwabagua na kuwanyanyapa

Chanzo:Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa