UPUNGUFU wa matundu ya vyoo katika shule za msingi za Halmashauri ya 
wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, imetajwa inaweza kusababisha mlipuko
 wa magonjwa kutokana na baadhi ya shule wanafunzi wake kujisaidia ovyo.
Akizungumzia changamoto hiyo, Mkuu wa wilaya hiyo Hawa Ng’humbi 
alisema wanaendelea kushirikiana na wadau kuhakikisha wanaondoa tatizo 
hilo.
Alikiri tatizo ni kubwa huku akibainisha kuwa matundu ya vyoo 
yaliyopo ni 693 ambapo mahitaji yao 1,257 hivyo kuwa na upungufu wa 564.
Alisema ili kuondoa upungufu huo, ushirikiano wa pamoja unahitajika 
baina ya wazazi na serikali kuwezesha wanafunzi kusoma katika mazingira 
mazuri yatakayokuwa rafiki kwao.
“Tunaendelea kuangalia jinsi ya kumaliza au kupunguza tatizo hili 
maana ni kero kubwa watoto wanalazimika kwenda vichakani au nyumba za 
jirani, ninaamini tukishirikiana tutafanikiwa,” alisema.
Kwa upande wake Ofisa Elimu Msingi , Sostenence Mbwilo alisema 
wameshaanza kufanyia kazi changamoto hizo kwa kushirikiana na wadau 
mbalimbali.
Chanzo Gazeti la Habari leo
  
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment