Home » » MBUNGE AZZA HILAL AWAPIGA JEKI WANAFUNZI WENYE ULEMAVU SHULE YA MSINGI ALIYOSOMA SHINYANGA

MBUNGE AZZA HILAL AWAPIGA JEKI WANAFUNZI WENYE ULEMAVU SHULE YA MSINGI ALIYOSOMA SHINYANGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.


Mbunge wa viti Maalum mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Azza Hilal (CCM) akikabidhi baiskeli kwa mwanafunzi mwenye ulemavu (hatembei wala haongei) katika shule ya msingi Tinde-Picha na Said Nassor-Malunde1 blog Tinde
Mbunge wa viti Maalum mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Azza Hilal (CCM) akikabidhi baiskeli kwa mwanafunzi mwenye ulemavu wa viungo katika shule ya msingi Tinde,aliyeshikilia kipaza sauti ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mheshimiwa Josephine Matiro.


Mbunge wa viti Maalum mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Azza Hilal (CCM) ametembelea shule ya msingi aliyosoma Tinde iliyopo katika kata ya Tinde wilaya ya Shinyanga kisha kutoa msaada kwa wanafunzi nane wenye ulemavu wa viungo akiwemo kijana ambaye hawezi kuongea wala kutembea. Mbunge huyo ametembelea shule hiyo jana Jumatano Septemba 27,2017. 

Mheshimiwa Hilal ametoa msaada wa baiskeli kwa kijana ambaye hawezi kutembea wala kuongea anayesoma katika shule hiyo huku akijitolea kuwanunulia wanafunzi hao nane mahitaji yao yote ya shule mpaka watakapomaliza masomo yao ya shule ya msingi. 

“Hii shule nimesoma,baada ya kufika hapa nimeambiwa kuna watoto wenye ulemavu,baada kumuona kijana huyu nimempatia baiskeli lakini pia nimejitolea kuwahudumia wanafunzi hawa wanane ambao wana ulemavu wa viungo,nitawanunulia mahitaji yao ya shule na watakuwa wanakunywa uji kila siku kwa gharama zangu”,ameeleza Mbunge huyo. 

Mbali na kutoa msaada huo Mheshimiwa Azza Hilal ameshiriki zoezi la Upandaji miti katika wilaya ya Shinyanga lililoanzishwa na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro lenye kauli mbiu ya "Shinyanga Mpya, Mti Kwanza". 

Akiwa katika kata ya Tinde,mbunge huyo aliungana na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro kupanda miti katika shule ya msingi Tinde,pia katika barabara kuu ya kutoka Tinde kwenda Kahama na barabara ya kutoka Tinde kwenda Nzega mkoani Tabora.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa