Home » » WATAKIWA WASIZIDHARAU SHULE ZA KATA

WATAKIWA WASIZIDHARAU SHULE ZA KATA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 
WITO umetolewa kwa watanzania kuacha kuzibeza shule za sekondari za kata badala yake waziamini na kuziunga mkono hasa kwa kuwa kipindi hiki ambapo shule hizo zinafanya vizuri katika mitihani ya kitaifa.
Mkuu wa shule ya sekondari Mwendakulima wilayani Kahama Shinyanga, Diana Kuboja alisema hayo alipowapongeza wanafunzi 15 kati ya 23 waliofaulu kidato cha sita kwa daraja la kwanza shuleni hapo.
Katika hafla hiyo iliyoandaliwa na Kampuni ya African Barrick Gold Mine (ABG) kupitia mgodi wake wa Buzwagi, Diana alisema matokeo ya mwaka huu kidato cha sita wanafunzi wote 23 wa shule yake wamefaulu kati yao nane walipata daraja la pili na waliobaki walipata daraja la kwanza.
“Mwendakulima imekua ya kwanza kimkoa na kikanda… kitaifa kwa shule zenye wanafunzi 180 imekuwa ya tisa, hivyo jamii inapaswa kuheshimu matokeo hayo,” alisema mkuu huyo wa shule.
Alisema serikali inajitahidi kuboresha mazingira ya ufundishaji kwa kuleta walimu wenye taaluma hivyo ni budi jamii nayo ikatoa msaada wa kuboresha mazingira ya miundombinu na majengo kwa kushirikiana na wafadhili hatua itakayozidisha hamasa ya kufanya vema kwa sekodari za kata.
“Si sahihi shule hizi kuziita yeboyebo na kauli hiyo ni changamoto kwetu kuuhakikishia umma kuwa tunaweza… jamii itambue ubora wa shule zetu,” alisema.
Mkuu wa Kitengo cha Sheria kutoka ABG na Mkurugenzi wa Bodi ya Ufadhili wa ‘Can Educate’ ya jijini London Uingereza, Katrina White alisema kampuni yake imeongeza Dola 5,000 za Marekani kwenye ufadhili katika huduma za jamii kwa maeneo jirani na migodi.
Meneja Mkuu wa mgodi wa Buzwagi, Philbert Rweyemamu ameitaka jamii kuwa mstari wa mbele katika suala zima la maendeleo kuliko kutegemea mgodi huku akibainisha kwamba mgodi wake umefadhili wanafunzi 400 wa shule za msingi katika kata hiyo wakati wanafunzi 200 wa sekondari wamepata ufadhili huo.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa