Home » » MIZANI FEKI 78 YA KUPIMIA PAMBA YAKAMATWA

MIZANI FEKI 78 YA KUPIMIA PAMBA YAKAMATWA


Na Isaack Mbwaga, Maswa
Jumla ya mizani 233 ya kupimia uzito wa pamba na mbegu katika wilaya za maswa na meatu imekaguliwa na maafisa wa vipimo katika mkoa wa shinyanga katika oparesheni maalumu ya kuhakikisha wakulima hawapunjwi wakati wa kuuza pamba yao.
Meneja wa Vipimo katika Mkoa wa Shinyanga Luppi Shirima alisema kati ya mizani hiyo aina rula, 155 baada ya kugaliwa zimekutwa ziko katika vipimo sahihi na kuruhusiwa kuendelea na kazi wakati mizani 78  imekutwa imeharibiwa  na watumishi wa makampuni yanayo nunua pamba kwa makusudi  kwa lengo la kuwaibia wakulima wanapo uza  pamba yao gulio
Shirima alisema mizani hizo zilikutwa zina wapunja wakulima kati ya kilo 12 hadi kilo 30 wakati wa kuuza pamba yao katika gulio
Meneja huyo alisema watu wote waliobainika kwa hujuma hiyo ya kuhujumu mizani ya kupimia pamba wametozwa faini kati ya shilingi 200,000/hadi 400,000/ kwa kila mizani iliyo kutwa imechakachuliwa
Hata hivyo alitoa onyo kwa  watu wanaoharibu mizani kwa makusudi sheria itachukua mkondo wake kwa wenye makampuni.
Serikali ilitoa maelekezo kwa makampuni yote yanayo nunua pamba mwaka huu kutumia mizani aina ya dijitali katika kupimia pamba katika vituo wakati wa kunua pamba katika vituo hivyo.
Blogzamikoa

0 comments:

 
Supported by Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa