Home » » WAHAMIAJI HARAMU 11 WATIWA MBARONIWAHAMIAJI HARAMU 11 WATIWA MBARONI

WAHAMIAJI HARAMU 11 WATIWA MBARONIWAHAMIAJI HARAMU 11 WATIWA MBARONI



na Stella Ibengwe, Shinyanga
WAHAMIAJI haramu 11 raia wa Ethiopia wanashikiliwa na Idara ya Uhamiaji mkoani Shinyanga kwa kosa la kuingia nchini kinyemela.
Raia hao walikamatwa jana wakiwa ndani ya mabasi tofauti wakitokea jijini Mwanza na kudai wanaelekea Tabora kwa ndugu zao.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kaimu Ofisa Uhamiaji wa Mkoa, Salumu Farahani, alithibitisha kukamatwa kwa raia hao na kueleza kuwa walikamatwa kwa nyakati tofauti wakiwa ndani ya mabasi mawili tofauti, likiwa basi la AM Coach linalofanya safari zake kati ya Mwanza na Tabora.
“Septemba 21 tuliwakamata raia nane na Septemba 23, tuliwakamata watatu na katika mahojiano wanaeleza kuwa wanakwenda kwa ndugu yao aliyeko Tabora na mpaka sasa tuna namba zake, lakini tukipiga simu yake haipatikani na wao wamekuwa sio wakweli kueleza kile kinachowapeleka huko,” alisema.
Aliwataja waliokamatwa kwenye basi la AM Coach kuwa ni Datun Suyubu, Tarkega Wadedebo na Teshal Heliso na wengine Bahiradia Ibrahimu, Hand Chafario, Muktar Nuriya, Tofke Gabir, Gatachawe Abute Chamso Hasawe, Tasfay Ayie na Muhba Gamali waliokamatwa kwenye basi lingine.
Alisema mbinu wanayoitumia kwa sasa wahamiaji hao ni kujiweka katika makundi madogo madogo na sio makubwa kama ilivyozoeleka na kupanda mabasi, ili kukutana sehemu ambayo wamepanga.
Chanzo: Tanzania Daima


0 comments:

 
Supported by Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa