Home » » BUNDI WAZUA TAFRANI MKUTANO WA CCM KAHAMA, WATUA MEZA YA LEMBELI, MGEJA, WAGOMA KUTOKA UKUMBINI, DIWANI ASEMA MATUKIO YA USHIRIKINA LAZIMA YAKEMEWE

BUNDI WAZUA TAFRANI MKUTANO WA CCM KAHAMA, WATUA MEZA YA LEMBELI, MGEJA, WAGOMA KUTOKA UKUMBINI, DIWANI ASEMA MATUKIO YA USHIRIKINA LAZIMA YAKEMEWE




Na Patrick Mabula, Kahama 

KATIKA hali ya isiyo ya kawaida Bundi wawili wameingia kwenye ukumbi wa mikutano kisha kutua meza kuu wakati wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilayani Kahama uliofanyika Shule ya Msingi Rocken Hill.

Kituko hicho kilitokea jana wakati ndege hao aina ya bundi walipotua katika meza waliyokaa Mbunge wa Jimbo la Kahama, Bw.James Lembeli na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Bw.Hamis Mgeja.

Mbali na kutua kwenye za watu hao ambao ni mahasimu kisiasa, pia waliendelea kukaa ukumbimbi wakati shughuli za uchaguzi zikiendelea hali iliyozusha hofu miongoni mwa wajumbe wa mkutano huo.

Shuhuda wetu alieleleza kuwa tukio hilo lilitokea wakati wajumbe wakijiandaa kuchagua viongozi wao, ndipo bundi ha wawili wawili waliingia kwenye ukumbi wa mikutano. Kitendo cha bundi hao kuvamia mkutano huo kiliwafanya wajumbe kutaharuki na kila mmoja  akitafasiri tukio hilo kwa mtazamo wake na wengine kulihusisha na imani za ushirikana.

Wakati wajumbe wakiwa wamekaa ukumbini ghafla bundi hao waliingia ukumbini na kisha waliruka hadi kwenye meza ya Bw. Lembeli na Bw. Mgeja, kisha kusababisha matafaruku mkubwa kwa wagombea nafasi mbali mbali.

Diwani wa Kata ya Chambo Bw.Damas Joseph, alisema mambo hayo  yanayodhaniwa kuwa ya  kishirikina katika chaguzi za CCM ni lazima yakemewe kwa vile yanawapa hofu mbalimbali na kuwafanya baadhi kutojiamini . 

Bw. Deo Ndimila tangu Kata ya Ukune alithibitisha vitendo vya kishirikina katika chaguzi za CCM mara nyingi zimekuwa zikitawala kwa baadhi ya watu kuendekeza imani hizo potofu.

Chanzo: Majira


0 comments:

 
Supported by Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa