MWANAMKE
mmoja aliyefahamika kwa jina la Kwezi Seleli (20) mkazi wa kijiji
cha Kalama,kata ya Uyogo wilayani Kahama mkoani Shinyanga ameuwawa
kwa kuchinjwa sehemu za shingoni na mume wake akiwa amelala usiku.
Kamanda
wa jeshi la polisi mkoani Shinyanga Evarist Mangalla amethibitisha
kutokea kwa tukio hilo leo saa kumi alfajiri katika kijiji hicho huku
akimtaja mwanamume aliyefanya mauaji hayo kuwa ni Chalia Samweli (25).
Kwa
mujibu wa Kamanda huyoa amesema kuwa mwanaume huyo alitumia panga
kumuua mke wake huku naye akifanya jaribio la kujia kwa kunywa sumu
aina ya Diazone inayotumika kuogeshea mifugo ambapo hakufa alikuwa
mahututi.
Aidha
kamanda amesema kuwa katika eneo la tukio kulikutwa panga moja na
kwamba chanzo cha tukio hilo bado kinachunguzwa na mtuhumiwa wa mauaji
hayo amelazwa katika hospitali ya wilaya ya Kahama kwa kupatiwa
matibabu.
CHANZO: DUNIA KIGANJANI BLOG
You might also like:
0 comments:
Post a Comment