SHULE ya Msingi Bugarama  ambayo ipo katika eneo linalozunguka Mgodi
 wa dhahabu wa Bulyanhulu  unaomilikiwa na Kampuni ya African Barrick 
Gold Mines Ltd imefungwa baada ya  kukosa vyoo.
  Mkaguzi Mkuu wa Shule  za Msingi wilayani Kahama, Ephraim Kaijuko, 
alisema jana kuwa shule hiyo  ilifunguwa juzi baada ya kubaini wanafunzi
 1,500 wanaosoma hapo hawana pa  kujisaidia na badala yake hujisaidia 
vichakani.
  Alisema idara yake sasa  inazunguka wilaya nzima kufanya ukaguzi wa 
mapungufu mbalimbali yaliyomo kwenye  shule za msingi huku kubwa zaidi 
likiwa ni vyoo.
  Wilayani Kahama idadi  kubwa ya shule za msingi hazina vyoo baada ya 
vilivyokuwepo kupitia mpango wa  MMEM kubomoka na vingine kuchakaa baada
 ya kujengwa chini ya kiwango.
  Aidha, katika mpango  huo wa MMEM hakukuwa na jitihada nyingine za 
ujenzi wa vyoo vingine licha ya  idadi ya wanafunzi kuongezeka kila 
mwaka na kufanya vilivyokuwepo kuzidiwa  matumizi.
Chanzo;Tanzania Daima 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment