Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja amesema chama
hicho kiko imara na kitaendelea hakuna mtu yeyote ndani na nje wa
kukiyumbisha.
Akifunga kampeni za uchaguzi wa udiwani kwa
nyakati tofauti vijiji vya Nonwe na Salawe, Kata ya Ubagwe, wilayani
Kahama juzi, Mgeja alisema CCM inaheshimika na itaendelea kuwa imara.
Mgeja aliwataka Watanzania kuachana na propaganda
na kutoyumbishwa na watu wasioitakia mema nchi, wanaokitabia kifo chama
hicho.
Alisema ndoto hizo za mchana hazina ubashiri
wowote, bali CCM ikpo imara na kitaendelea kuwa imara kwani kinafanya
vizuri katika ngazi zote. CCM imemsimamisha Khamis Majogoro Mbogola
kwenye uchaguzi huo mdogo uliofanyika.
“Hivyo kitaendelea kuwa imara na hakuna mtu yeyote ndani na nje ya chama atakayekiyumbisha,” alitamba Mgeja.
Alisema chama hicho na jumuiya zake zinafanya kazi
vizuri kusimamia ilani yake ya Uchaguzi ya mwaka 2010 hadi 2015, chini
ya Mwenyekiti wake, Jakaya Kikwete.
Mgeja alikumbusha maneno ya Baba wa Taifa, Hayati
Mwalimu Julius Nyerere kuwa, ili maendeleo yapatikane vinahitajika vitu
vitatu; Watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora ambavyo vinapatikana
CCM.
“Ndiyo kazi na malengo tangu tunadai na uhuru
wetu hadi sasa, CCM na Serikali yake vinasimamia misingi hiyo vizuri
japo kuna watu wachache wanafanya kwa maslahi yao, wala CCM
haijawatuma,” alisema Mgeja.
Pia, aliwaomba wananchi kuichagua CCM kwani ndicho chama pekee ambacho ni mwarobaini wa kutatua matatizo yao.
“Nawaomba mpime tofauti yetu na vyama vya
upinzani hasa Chadema, CCM inahubiri amani, umoja na mshikamano wa
kitaifa, wakati wenzatu walishaapa nchi haitatawalika nyinyi ni
mashahidi na mnayaona matukio mbalimbali ya vurugu yanayofanywa
nchni,”alisema Mgeja
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment