Home » » Ahadi ya Serikali kwa wakazi wa Mwakata bado Kitendawili

Ahadi ya Serikali kwa wakazi wa Mwakata bado Kitendawili

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Wakazi wa Mwakata wilayani Kahama Mkoani Shinyanga bado wanakubwa na kadhia ya kukosa makazi baada ya kukubwa na mvua ya mawe iliyoua watu 42 na na kujeruhi 91 mwaka jana 2015 mwezi marchi.

Hayo yamebainishwa Bungeni na Mbunge wa Msalala Ezekiel Maige (CCM) alipokuwa akichangia hotuba ya Rais Dkt. John Magufuli katika ukumbi wa Bunge mjini Dodoma.

Mheshimiwa Naibu Spika Baada ya maafa yale kutokea Rais aliyepita Jakaya Kikwete aliagiza wananchi wale wajengewe nyumba za kuishi ndani ya muda mfupi lakini hadi tunavyozungumza wananchi wale wanaishi kwenye maturubali jambo ambapo sii sahihi.

''Ahadi ya Serikali ni ahadi ambayo inahitaji utekelezaji hivyo namuomba ndugu yangu Jenista Mhagama Bunge likimalizika twende pamoja jimboni ukajionee hali halisi ili serikali muanze kuwajengea nyumba wananchi hawa maana wanateseka na mvua zinazoendelea kunyesha.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa