Home » » JITOKEZENI KWA WINGI WIKI YA SHERIA - DC

JITOKEZENI KWA WINGI WIKI YA SHERIA - DC

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MKUU wa Wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro ametoa mwito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi wakati wa kutoa elimu katika vyombo vinavyosimamia haki na sheria.
Amesema hatua hiyo, itawawezesha kufahamu haki inapotendeka na kuondoa manung’uniko, yanayotokea mara kwa mara katika vyombo hivyo.
Aliyasema hayo jana wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria, yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Zimamoto Manispaa ya Shinyanga.
Aliwataka kujitokeza kusikiliza elimu, inayotolewa katika makundi ya Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), Jeshi la Polisi na Mahakama.
“Mahakama kushirikiana na wadau wanatakiwa kupunguza kesi ikiwa magerezani kuna malalamiko mengi na masomo ya kufahamu sheria mbalimbali au kutembelea maeneo ya magereza yawe endelevu ili kuweza kuondoa changamoto zilizopo hasa zinazoelezwa na wananchi,” alisema Matiro.
Ofisa Mradi wa Ulinzi wa Mtoto kutoka shirika linalojihusisha na msaada wa kisheria (Paceshi), Shadia Nurdin aliyehudhuria maadhimisho hayo, alisema mpaka sasa kuna kesi 40 zinazoendelea katika Mahakama ya Wilaya hadi Mahakama Kuu na kesi 10 zimekwishatolewa hukumu, ila zinazoongoza ni zile za masuala ya ardhi na mirathi.
Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Shinyanga, Sekela Mwaiseje alisema uzinduzi wa wiki ya elimu ya sheria ni kutoa fursa kwa wananchi kutambua haki zao kwa utaratibu ikiwemo mwenendo wa kesi za mirathi na ardhi.
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Shinyanga, Rahimu Mushi alisema wananchi wengi wamekuwa wakilalamika kutotendewa haki na Mahakama, chanzo ni wao kutokuwa na elimu, hivyo sasa wameamua kushirikisha wananchi na wadau ili kuwapatia elimu.
CHANZO ; HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa