Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MKURUGENZI Mtendaji wa Manispaa ya Shinyanga, Lewis Kalinjuna 
amezifunga baadhi ya kumbi za starehe na baa ya Dragoni iliyokuwa karibu
 na Shule ya Msingi Town kwa madai kuwa zimekosa viwango vinavyotakiwa 
ikiwemo kukosa huduma za vyoo.
Licha ya changamoto hiyo, katika shule hiyo ya msingi ndani ya 
madarasa kumekuwa mara kwa mara kukutwa na kondomu ambazo zimekwisha 
tumika hali ambayo ni hatari kwa wanafunzi.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, mkurugenzi huyo 
alisema klabu za usiku za Bakurutu maarufu Maduka Mengi, Lubaga Inn na 
Butiama zimefungwa mpaka zitakapojirekebisha kwa kutengeneza huduma 
zinazotakiwa.
Kalinjuna alisema baa ya Dragon imefungwa moja kwa moja kutoa huduma 
kwa sababu ya kutokukidhi viwango hasa kukosa huduma za vyoo na kuwa 
karibu ya eneo la shule.
“Hizi baa za usiku zinazokesha zimekuwa na changamoto nyingi hivi 
sasa ni suala la usafi kila maeneo wao wanaendesha biashara hizo 
pasipokuwa na huduma za vyoo. 
Tumeamua kuchukua hatua ya kuwasimamisha 
wasitoe huduma mpaka pale watakapojirekebisha ila baa ya Dragon yenyewe 
tumeifungia moja kwa moja,” alisema.
Mkurugenzi wa baa ya Dragon, Humprey Godfrey alisema kitendo cha 
kufungiwa kimemsikitisha kwani wakati akianza kufanya biashara hiyo 
alipewa leseni kutoka manispaa na kukagua mandhari yake sasa imekuwaje 
leo kufungiwa moja kwa moja hilo suala hawajatenda haki.
“Mimi nimeshangazwa na manispaa hii ina maana hawakuona kipindi 
wanaponipatia leseni kuwa nipo karibu na shule. Sasa nimeanza biashara 
wamekuja kunifungia kwa kueleza makosa mengi hivyo hawajanitendea haki,”
 alilalama mkurugenzi huyo.CHANZO: GAZETI LA HABARI LEO.
 

 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment