Home » » MABOSI ACACIA WANG’ATUKA

MABOSI ACACIA WANG’ATUKA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Imeandikwa na Mwandishi Wetu
Ofisa mtendaji mkuu wa kampuni ya Acacia, Brad Gordon na ofisa mkuu wa fedha Andrew Wray wamejiuzulu, kampuni hiyo ya uchimbaji wa madini imetangaza leo.
Kampuni hiyo yenye migodi mitatu ya dhahabu kaskazini magharibi mwa Tanzania imetangaza kuwa wawili hao wataondoka rasmi Acacia mwishoni mwa mwaka huu. Hata hivyo, taarifa inayopatikana kwenye tovuti ya kampuni imeeleza kuwa, Peter Geleta ataiongoza kampuni hiyo katika kipindi cha mpito huku Jaco Maritz akiongoza kitengo cha fedha.
Wateule hao wataanza kazi kuanzia Januari 1, mwaka kesho. Akizungumzia kujiuzulu kwa Brad na Andrew, mwenyekiti wa Acacia, Kelvin Dushnisky amenukuliwa na taarifa hiyo akisema, “Brad na Andrew wamekuwa kiungo muhimu katika uendeshaji na masuala ya fedha hapa Acacia kwa kipindi cha zaidi ya miaka minne. Kwa niaba ya bodi, ninapenda kuwashukuru kwa mchango wao kwenye kampuni. Tunawatakia kila la heri kwa siku za usoni.”
CHANZO HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Shinyanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa